NNAPE AWATETEA UVCCM BAADA YA KUCHAPANA MAKONDE


Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alisema kuwa Watanzania hawapaswi kushangazwa na kitendo cha vijana wa UVCCM kuchapana makonde juzi hadharani kwani tukio hilo si la kwanza kutokea kwao.

Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu, Nape alisema ugomvi wa juzi katika makao makuu ya umoja huo jijini Dar es Salaam ni mambo yanayowakuta vijana wengi katika maeneo mbalimbali na kwamba kinachotakiwa ni namna ya kuutuliza.
“Mimi niko Mwanza, sijapata taarifa sahihi hivyo siwezi kukupa tathmini yangu, lakini tambua haya yalianza enzi za kina John Guninita, hata mimi na Nchimbi tulishawahi kugombana mwaka 2003 kwa sababu ya umoja huo, cha msingi ni kuangalia nini kitafanyika baada ya tendo hilo,” alisema Nape.

Alisema wakati wa kina Guninita kanuni za uchaguzi zilifuatwa na bado kulitokea hali ya kutoelewana na kusisitiza kuwa hata marehemu baba yake Moses Nnauye akiwa kiongozi wa jumuiya hiyo, walishachapana kwa bakora kwa ajili ya kuweka mambo sawa.
Aliongeza kuwa anasikitishwa na hali ya vijana wa chama hicho kukosa uvumilivu hata kufikia hatua ya kuvamiana mwilini na kupigana na kwamba chama kitakaa baada ya kupata taarifa kamili na kisha kutoa tamko lake juu ya tukio hilo.

Tanzania Daima
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII

Copyright © 2013. ArtAfropixels Media.com - All Rights Reserved
Customized by: IT XPERTTZ ONE | Powered by: BS
Designed by: Tilabs