UMEISOMA HII?? DOGO JANJA ATIMULIWA MTANASHATI ENTERTAINMENT
Msanii mdogo aliyewahi
kutamba katika tasnia ya muziki wa bongo fleva Dogo Janja amefukuzwa
rasmi Mtanashati Entertinment, Taarifa zilizofikia dawati letu la habari
zinasema Dogo Janja amefukuzwa na Ostazi Juma Na Musoma baada ya
kushindwana kitabia, Hapo awali Dogo Janja aliwahi kuwa mwanakundi la
Tip Top Connection lililo chini ya uongozi wa Madee hata hivyo
alifukuzwa na kurudi kwao Arusha ambapo Ustazi Juma Na Musoma alimfuata
na na kumuweka kundini huku akimuhudumia katika kila jambo ambalo
alitakiwa kupata kama mtoto na mwanamuziki pia. Lakini Leo imefika
tamati ya Ostazi Juma na kuamua kumuacha Dogo Janja aende zake.
0 comments:
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII