AIBU : JACK WOLPER ATUPIWA VITU NJE BAADA YA KUSHINDWA KULIPA KODI YA NYUMBA...PATA UDAKU WOTE HAPA
Jacqueline Wolper Massawe.
STAA wa filamu za Kibongo, 
Jacqueline Wolper Massawe anadaiwa kutupiwa nje na baadaye kuzuiliwa 
vyombo vyake kwenye ile nyumba ya kifahari ya kupanga aliyokuwa akiishi 
Mbezi Beach, Dar es salaam.
Madai hayo yalitua kwenye dawati la 
GPL hivi karibuni ambapo ilielezwa kuwa ishu hiyo ilijiri maeneo hayo 
baada ya bishosti huyo kudaiwa kuwa alishindwa kulipa kodi ya pango ya 
mwezi mmoja ambayo ni Dola 1,500 (zaidi ya Sh. milioni 2.4 za madafu).
Kwa mujibu wa ‘sosi’ wetu 
aliyekuwepo eneo la tukio, Wolper aliwatuma ndugu zake kwenda kuchukua 
vyombo hivyo lakini walipofika mama mwenye nyumba (jina tunalo), 
aliwazuia na kumpigia simu staa huyo akimwambia kuwa anatakiwa kulipa 
fedha kabla ya kuchukua vitu vyake.
“Wolper alipopigiwa simu alikuja juu
 na kumwambia mama mwenye nyumba kuwa kama anamfuatilia eti atamfunga 
kama mume wa mama huyo alivyofungwa na kumwambia kuwa atampelekea polisi
 wakamkamate,” alidai mtu huyo.
Sosi huyo aliendelea kudai kuwa 
baada ya kuona soo limekuwa la kutishana, mama huyo alikwenda kumfuata 
mjumbe wa nyumba kumi aliyefahamika kwa jina moja la Musa na kumueleza 
kisha kumuomba asimamie zoezi hilo.
Baada ya kujazwa data hizo, GPL 
ilifanya jitihada za kumsaka Wolper na alipopatikana alisema kuwa 
hajawahi kudaiwa na huyo mama na anayesema hivyo huenda alimuona wakati 
anahamisha vitu vyake kwani kwa sasa amehama kwenye nyumba hiyo.
Mwandishi wetu hakuishia hapo, 
alimtafuta shemeji wa mama mwenye nyumba aliyetajwa kwa jina moja la 
Jamal ambaye alikiri kutokea kwa ishu hiyo na kwamba suala hilo 
lilimalizika ambapo vyombo vya Wolper vilitolewa kwa ajili ya kufanya 
usafi kwani kuna mtu mwingine alikuwa akihamia.
Mjumbe wa Nyumba Kumi, Musa 
alipotafutwa kwenye simu yake ya kiganjani ili kuzungumzia sakata hilo 
alikiri kufikishiwa malalamiko ya Wolper.
Alisema kuwa msanii huyo alikuwa 
hajamaliza kulipa fedha, akawatuma ndugu zake wakachukue vitu vyake 
lakini kabla hawajavichukua mama mwenye nyumba aliwazuia mpaka alipwe 
chake na alipotimiza hilo ndipo akaachiwa vitu vyake
 
 
 
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII