Showing posts with label siasa. Show all posts

HIVI NDIVYO M4C ILIVYOKULA VICHWA MOROGORO, AFANDE SELE NAYE ALIHUTUBIA

0 comments

Halima Mdee: Mbunge wa Kawe, Halima Mdee akiwahutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Mtibwa, katika mkutano wa Operesheni M4C Pamoja Daima, uliofanyika jana.
Mbowe na Afande Sele: Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akimtambulisha mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya, Afande Sele, wakati wa mkutano wa Operesheni M4C Pamoja Dama, uliofanyika katika Kata ya Tungi mjini Mororgoro jana.
Afande Sele: Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya, Afande Sele akiwahutubia wananchi wa Kata ya Tungi mjini Morogoro jana, katika mkutano wa hadhara wa Operesheni M4C Pamoj Daima, ambao pia ulihutubiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe.
Mbowe, Halima wakiondoka Ifakara: Mwenyekiti wa Chama cha Demokreasia na Maendeleo (CHADEMA) na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee wakiondoka baada ya kuhutubia mkutano wa Operesheni M4C Pamoja Daima, uliofanyika mjini Ifakara jana.
Mkutano Ifakara: Maelefu ya wakazi wa mji wa Ifakara, wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wa Operesheni M4C Pamoja Daima, ambao ulihutubiwa na Mweneyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) jana.
Mabango Ifakara: Baadhi ya wananchi mji wa Ifakara wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe mbalimbali, wakati wa mkutano wa Operesheni M4C Pamoja Daima, ambao ulihutubiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe jana.

Wananchi Ifakara: Sehemu ya maedlfu ya wakazi wa mji wa Ifakara, wakitawanyika baada ya mkutano wa Operesheni M4C Pamoja Daima, ambao ulihutubiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe jana.
(Picha na JF)

Soma zaidi Hapa »

BREAKING NEWS : KIKWETE ATANGAZA BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI, HAYA NDIO MAJINA YA BARAZA JIPYA, BOFYA HAPA

0 comments

Mabadiliko Baraza la Mawaziri 2014


Soma zaidi Hapa »

HUU NDIO UTETEZI ALOUTOA ZITTO KWA KAMATI KUU, USOME HAPA

0 comments
 
Mh.zitto Kabwe




Our Ref: ZZK/12/13 10.12. 2013.Mh. Katibu MKuu, Chama Cha Demokrasia Na Mendeleo HSE NO 170,
UFIPA STREET, KINONDONI 
S. L. P 31191 Dar es Salaam – Tanzania. 
YAH: MASHATAKA YA UKIUKWAJI WA KATIBA, KANUNI NA MWONGOZO WA CHAMA.

Rejea barua yako ya tarehe 26 Novemba 2013 yenye kumbukumbu no C/HQ/ADM/KK/08/31 Iliyoelezea maamuzi yaliyofikiwa na kikao cha Kamati Kuu ya Chama cha tarehe 20-22 Novemba 2013, kiliazimia kwamba niachishwe nafasi zote za uongozi ninazoshikilia katika chama na kwamba Kamati Kuu iliazimia kwamba hatua zaidi za kinidhamu za kuachishwa ama kufukuzwa uanachama zichukuliwe dhidi yangu kwa mujibu wa Katiba na Kanuni za Uendeshaji za 6.5.2(d), ningependa kuwasilisha majibu ya mashtaka hayo kama ifuatavyo; 
1.0 MAELEZO YA AWALI;Napenda kuwasilisha utetezi wangu huku nikiwa napinga utaratibu uliotumika kuandaa na kunifikishia mashtaka husika (Defence Under Protest) kwa sababu zifuatazo; 
1.1. Hatua za kinidhamu ambazo kimsingi ni adhabu zimeshachukuliwa na Kamati Kuu kwa mashtaka haya haya ambayo nimepatiwa. Kama barua yako inavyosema na nanukuu maneno yako “Kamati Kuu kwa kutumia mamlaka yake kwa mujibu wa Kanuni ya 6.5.2(d) ya Kanuni za Uendeshaji Shughuli za Chama (‘Kanuni za Uendeshaji’), iliazimia kwamba muachishwe nafasi zote za uongozi mnazoshikilia katika Chama…” (msisitizo ni wangu).Mheshimiwa Katibu Mkuu;Ni wazi kabisa kwamba adhabu ya kuachishwa nafasi zote za uongozi imeshatekelezwa. Kamati Kuu imeshanitia hatiani kwa makosa haya haya ambayo sasa hivi natakiwa nijitetee. Binafsi siamini kwamba kwa utaratibu huu haki itatendeka na inaonekana kutendeka. Ni vigumu sana kusema kwamba haki yangu ya msingi ya kusikilizwa na kujitetea imelindwa wakati tayari adhabu imeshatolewa na chombo kile kile ninachotakiwa kujitetea mbele yake. 
1.2. Kama kiongozi ambaye nimeadhibiwa na Kamati Kuu ninayo haki ya kukata rufaa Baraza Kuu dhidi ya haya yafuatayo; 1.2.1. utaratibu uliotumika na Kamati Kuu kunivua nyadhifa zote za uongozi. 1.2.2. sababu zilizotumika kunivua nyadhifa zote za uongozi. 
Mheshimiwa Katibu Mkuu; 
Katiba ya Chama pamoja na Kanuni za Uendeshaji zinatoa HAKI hii ya msingi na UTARATIBU kwa maneno haya; 
Ibara 6.3.6(d) ya Katiba ya Chama;“Kiongozi aliyechukuliwa hatua za kinidhamu na mamlaka yake ya nidhamu anayo haki ya kukata rufaa ngazi ya juu ya ile mamlaka yake ya nidhamu na uamuzi wa ngazi hiyo utakuwa wa mwisho”. 
Ibara 6.3.6(e) ya Katiba ya Chama;“Rufaa yoyote lazima ifanyike katika muda wasiku thelathini tangu tarehe ya kupokea rasmi kwa maandishi maamuzi ya mamlaka iliyotoa adhabu”.Mheshimiwa Katibu Mkuu;Kanuni za Uendeshaji zinatoa UTARATIBU ambao unatakiwa ufuatwe ili kiongozi aliyeadhibiwa aweze kutumia HAKI yake ya kukata rufani kwa maneno haya;Kanuni ya 6.5.8 ya Kanuni za Uendeshaji;“Kiongozi aliyeadhibiwa atapewa taarifa ya msingi wa maamuzi ya mamlaka ya nidhamu ili kumuwezesha kuamua kukata rufani au la” 
Kanuni ya 6.5.9 ya Kanuni za Uendeshaji;“Mwadhibiwa atakayeamua kukata rufani atatakiwa kufanya hivyo katika muda wa siku thelathini baada ya kuarifiwa uamuzi wa adhabuKanuni ya 6.5.10 ya Kanuni za Uendeshaji;“Baada ya kutoa uamuzi kikao husika kinalazimika kuandaa taarifa kamili ya mwenendo wa shauri na kuwasilisha ngazi ya juu. Taarifa hiyo lazima ifike katika muda wa siku kumi na nne baada ya kikao cha mamuzi Mheshimiwa Katibu Mkuu; Mpaka tarehe 01/12/2013 siku ambayo nimepokea barua yako ya mashtaka dhidi yangu sijapokea taarifa ya msingi wa maamuzi ya mamlaka ya nidhamu na pia taarifa kamili ya mwenendo wa shauri langu haujawasilishwa Baraza Kuu. Wakati hayo yote hayajafanyika natakiwa kutoa utetezi wangu wa maandishi kwa mujibu wa Kanuni ya 6.5.2(a) ikisomwa pamoja na Kanuni ya 6.5.6 ya Kanuni za Uendeshaji kwa makosa yaleyale ambayo tayari nimeshaadhibiwa na Kamati Kuu. Ni wazi kabisa kwamba barua yako ya mashtaka ni muendelezo wa hatua au maazimio ya Kamati Kuu kama ilivyoandikwa “Aidha Kamati Kuu iliazimia kwamba hatua zaidi za kinidhamu za kuachishwa ama kufukuzwa uanachama zichukuliwe….” 
Mheshimiwa Katibu Mkuu; 
Utaratibu uliotumika na Kamati Kuu sio wa HAKI na ni ukiukaji wa Katiba na Kanuni za Uendeshaji. Nalazimika kutoa utetezi wangu nikiwa napinga (under protest) kwa sababu kwa Chama ambacho kinasifika kwa kupigania misingi ya utawala bora na utawala wa sheria ni lazima kiheshimu haki za wanachama na viongozi wake pamoja na kufuata utaratibu kilichojiwekea wakati wa kuchukua hatua za kinidhamu.1.3. Baadhi ya wajumbe wa Kamati Kuu kwa nyakati mbalimbali wametoa matamko kwamba tumefukuzwa uongozi na hatua zaidi zitachukuliwa dhidi yetu kabla hata ya ofisi yako kutoa Mashtaka dhidi yetu. Mheshimiwa Tundu Lissu na Mheshimiwa John Mnyika walitoa matamko hayo wakati wakiongea na Waandishi wa Habari. Mheshimiwa Katibu Mkuu; 
Kitendo cha wajumbe hao kutoa misimamo kwa niaba ya Chama au Kamati Kuu ni ukiukwaji wa haki yangu ya msingi ya kusikilizwa. Ni wazi kabisa kwamba tayari hukumu dhidi yangu imeshapitishwa kabla sijasikilizwa. Sina imani na wajumbe ambao tayari wameonyesha waziwazi misimamo yao kuhusu tuhuma dhidi yangu. Mheshimiwa Katibu Mkuu; 
Kutokana na hayo yote ambayo nimeyataja hapo juu naomba ofisi yako isitishe utekelazaji wa maamuzi au maazimio ya Kamati Kuu mpaka pale ambapo nitakuwa nimepatiwa taarifa ya msingi wa maamuzi ya Kamati Kuu na kuweza kukata rufaa ngazi ya juu kwa mujibu wa Katiba na Kanuni za Uendeshaji. Hatua zozote za Kamati Kuu zitaendelea kukiuka Katiba na Kanuni za Uendeshaji. 
Bila kuathiri hayo niliyoyasema; 
UTETEZI WANGU DHIDI YA MASHTAKAMheshimiwa Katibu Mkuu;Kwa ujumla nakanusha na kukataa kuhusu tuhuma zinazoelekezwa kwangu kuhusu kinachoelezwa kwamba niliandaa mkakati wa mabadiliko 2013, mimi binafsi sijawahi kushiriki, kuhusika kuandaa au kufahamu kwa namna yoyote ile kinachoitwa waraka wa Mkakati wa Mabadiliko 2013 kama ulivyoainisha kwenye barua yako. KOSA LA KWANZA 
Kukashifu Chama kiongozi au mwanachama yeyote wa chama kinyume na masharti ya 10.1(xii) ya Kanuni za UendeshajiMheshimiwa Katibu Mkuu; 
1. Nakanusha kwamba mimi pamoja na Dk. Kitila Mkumbo, Bw. Samson Mwigamba na Mtu mwingine ambaye hajajulikana niliandaa waraka ulioitwa Mkakati wa Mabadiliko 2013. 2. Sijawahi kushiriki kwa njia yoyote kuandaa waraka huo peke yangu au nikiwa na mtu mwingine yeyote. Nakanusha kumkashifu Mwenyekiti wa Chama Taifa kwa njia yoyote ile. 
3. Kuhusu kutoa kashfa kwa Katibu Katibu Mkuu wa Chama na Mbunge wa Arusha Mjini Mh. Godbles Lema kama ulivyoainisha kwenye barua yako mimi binafsi sijawahi kutoa kashfa hizo na wala kuhusika kwa namna yoyote ile kwenye maandalizi ya mkakati huo wa mabadiliko.

KOSA LA PILI
Kutokuwa wakweli na wawazi wakati wote na kushirikiana na vikundi vya majungu na wadanganyifu (rumour mongers) Kinyume na Kanuni ya Uendeshaji 10.1 (vii) ya Kanuni za Uendeshaji.Mheshimiwa Katibu Mkuu; 
1. Nakanusha kwamba mimi pamoja na Dk. Kitila Mkumbo, Bw. Samson Mwigamba na Mtu mwingine ambaye hajajulikana nilianzisha mtandao wa siri ulioitwa “Mtandao wa Ushindi’ ili kuniwezesha mimi kutwaa madaraka ya Mwenyekiti wa Chama Taifa kwa njia zilizo kinyume na Katiba, Kanuni za Uendeshaji na Kanuni za Kusimamia Shughuli, Mwenendo na Maadili ya Wabunge wa CHADEMA na Mwongozo wa Kutangaza Kusudio la Kuwania Nafasi za Uongozi Kwenye Chama, Mabaraza na Serikali 2012. 2. Nakanusha kuanzisha, kushiriki uanzishwaji au kuufahamu unaoitwa mtandao wa ushindi kama ilivyoelezwa na barua yako. 3. Siku zote nimekuwa mkweli muwazi kwa yale ninayoyaamini na katika kutekeleza majukumu yangu kama kiongozi na mwanachama mtiifu wa CHADEMA. Pia sijashirikiana na kikundi chochote cha majungu au wadanganyifu kama iliyoainishwa kwenye barua yako. 
KOSA LA TATU
Kutoa tuhuma juu ya viongozi wenzenu pasipo kupitia vikao halali na kuzingatia taratibu na ngazi zilizowekwa kwenye Kanuni kinyume na Kanuni ya 10.1(x) ya Kanuni za Uendeshaji.Mheshimiwa Katibu Mkuu; 
1. Nakanusha kwamba mimi pamoja na Dk. Kitila Mkumbo, Bw. Samson Mwigamba na Mtu mwingine ambaye hajajulikana nilitoa tuhuma nzito na za uongo dhidi ya viongozi wakuu wa Chama, yaani Mwenyekiti wa Chama Taifa na Katibu Mkuu pasipo kupitia vikao halali na bila kuzingatia taratibu na ngazi zilizowekwa na Kanuni za Uendeshaji. 2. Sijawahi kushiriki kwa njia yoyote kuandaa waraka huo peke yangu au nikiwa na mtu mwingine yeyote. Nakanusha kwamba nilitoa tuhuma nzito na za uongo dhidi ya viongozi wakuu wa Chama, yaani Mwenyekiti wa Chama Taifa n Katibu Mkuu pasipo kupitia vikao halali na bila kuzingatia taratibu na ngazi zilizowekwa na Kanuni za Uendeshaji.

KOSA LA NNE
Kujihusisha na vikundi vyenye misingi ya ukabila, udini, au ukanda ambavyo vina makusudi ya kubaguana ndani ya chama na miongoni mwa jamii kisiasa au kijamii na Kanuni ya 10.1(iv) ya Kanuni za Uendeshaji.Mheshimiwa Katibu Mkuu; 
1. Nakanusha kwamba nimejihusisha katika kuanzisha, kushiriki uanzishwaji au kufahamu kikundi chochote chenye misingi ya ukabila, udini, au ukanda ambacho kina makusudi ya kubaguana ndani ya chama na miongoni mwa jamii kisiasa au kijamii kwa kutumia waraka unaosemekana kuandaliwa nami. 
2. Mimi binafsi sio mdini, mkabila au mkanda na sijawahi kujihusisha na kikundi au mtu yeyote mwenye tabia hizo.

KOSA LA TANO
Kujihusisha na vikundi na vitendo vya kuchonganisha au kuzua migogoro ndani ya uongozi wa chama au wanachama wake na kinyume na Kanuni ya 10.1 (x) ya Kanuni za Uendeshaji.Mheshimiwa Katibu Mkuu; 
1. Nakanusha kwamba nimejihusisha na vikundi na vitendo vya kuchonganisha au kuzua migogoro ndani ya uongozi wa chama au wanachama wake. 
2. Mimi binafsi sikifahamu kikundi chochote ambacho nashutumiwa kujihusisha nacho.
KOSA LA SITA
Kutekeleza mpango wa kusudio la kugombea nafasi ya mwenyekiti wa Chama Taifa bila kutangaza kusudio la kugombea nafasi hiyo kinyume na kifungu cha 2(g) cha Mwongozo wa Kutangaza Kusudio la Kuwania Nafasi za Uongozi Kwenye Chama, Mabaraza na Serikali 2012.Mheshimiwa Katibu Mkuu; 
1. Nakanusha kwamba nimetekeleza au kuhusika katika utekelezaji wa mpango wa kusudio la kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Chama Taifa bila kutangaza kusudio la kugombea nafasi hiyo. 
2. Sijatangaza sehemu yeyote kwamba nitagombea nafasi hiyo na pia vile vile sijatekeleza mpango wowote kama ilivyoelezwa kwenye barua yako.
KOSA LA SABA
Kutengeneza makundi au mitandao ya kuwania uongozi ndani ya chama kwa nia ya kujihakikisha ushindi kinyume nakifungu cha 2(d) cha mwongozo wa kuwania uongozi.Mheshimiwa Katibu Mkuu; 
1. Nakanusha kwamba nimejihusisha katika kutengeneza, kuanzisha, kushiriki uanzishwaji au kufahamu kikundi chochote kwa ajili ya kuniwezesha kuwania uongozi ndani ya chama na kujihakikishia ushindi kutwaa Uenyekiti wa Chama Taifa kinyume na taratibu.

KOSA LA NANE
Kuwachafua viongozi na wanachama wengine wenye kusudio/nia ya kutaka kugombea nafasi ya Uenyekiti wa Chama Taifa kinyume nakifungu cha 2(e) cha Mwongozo wa Kuwania Uongozi.Mheshimiwa Katibu Mkuu; 
1. Nakanusha kwamba mimi pamoja na Dk. Kitila Mkumbo, Bw. Samson Mwigamba na Mtu mwingine ambaye hajajulikana niliandaa waraka ulioitwa Mkakati wa Mabadiliko 2013. 2. Sijawahi kushiriki kwa njia yoyote kuandaa waraka huo peke yangu au nikiwa na mtu mwingine yeyote. Nakanusha kumkashifu Mwenyekiti wa Chama Taifa, kiongozi mwenzangu au mwanachama yeyote Yule.

KOSA LA TISA
Kujihusisha na upinzani dhidi ya Chama na makundi ya majungu ya kugonganisha viongozi na wanachama wakati wa Uchaguzi wa Chama kinyume na Kanuni ya 10.3(4) ya Kanuni za Uendeshaji.Mheshimiwa Katibu Mkuu; 
1. Nakanusha kwamba mimi pamoja na Dk. Kitila Mkumbo, Bw. Samson Mwigamba na Mtu mwingine ambaye hajajulikana niliandaa mkakati wa kugonganisha viongozi na wanachama wakati wa Uchaguzi wa Chama kwa kuwachafua viongozi wakuu wa Chama yaani Mwenyekiti wa Chama Taifa na Katibu Mkuu kwa tuhuma nzito za uongo na kunipamba mimi. 2. Sijawahi kushiriki kwa njia yoyote kuandaa waraka huo peke yangu au nikiwa na mtu mwingine yeyote.

KOSA LA KUMI
Kukashifu Chama au Kiongozi wa Chama nje ya Bunge kinyume na Kanuni 2(b) ikisomwa pamoja na Kanuni 3(b) ya Kanuni za Mwenendo na Maadili ya Wabunge.Mheshimiwa Katibu Mkuu; 
1. Nakanusha kwamba mimi pamoja na Dk. Kitila Mkumbo, Bw. Samson Mwigamba na Mtu mwingine ambaye hajajulikana kwa kuandaa na kutumia waraka uitwao Mkakati wa Mabadiliko 2013 nilitengeneza mtandao haramu ndani ya Chama na nilitoa kashfa, matusi na uzushi dhidi ya Chama na viongozi wake wakuu kwa lengo la kuchochea mgawanyiko ndani ya Chama. 
2. ambao ulikashifu Chama na/au viongozi wake wakuu nikiwa Mbunge wa CHADEMA na Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni. 3. Sijawahi kushiriki kwa njia yoyote kuandaa waraka huo peke yangu au nikiwa na mtu mwingine yeyote. Nakanusha kwamba nimekashifu Chama au viongozi wake wakuu nikiwa Mbunge wa CHADEMA na Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni kwa njia yoyote ile.

KOSA LA KUMI NA MOJA
Kuchochea mgawanyiko ndani ya Chama kinyume na Kanuni ya 3(f) ya Kanuni za mwenendo na maadili ya Wabunge.Mheshimiwa Katibu Mkuu; 
1. Mimi kama kiongozi wa Kitaifa sijawahi kutengeneza mtandao haramu ndani ya Chama wala kutoa lugha ya matusi na uzushi dhidi ya Chama na viongozi wake wakuu kwa lengo la kuchochea mgawanyiko ndani ya Chama. 
HITIMISHO: 
Mheshimiwa Katibu Mkuu; 
a) Nakanusha kila tuhuma mojamoja na kwa ujumla wake dhidi yangu. Mashtaka yote dhidi yangu sio kweli na sijavunja Katiba au Kanuni za Chama. b) Naiomba Kamati Kuu ijiridhishe kwa kiasi kinachostahili kuhusu mashtaka yote niliyoshtakiwa nayo kwa kuangalia ushahidi wote uliotolewa au utakaotolewa dhidi yangu. c) Utetezi wangu umetolewa bila kupewa nakala ya Waraka unaosemekana nimeuandaa ilhali kukiwa na maelezo kwamba kuna waraka ‘feki’ na waraka ‘original’ ambao umetumika na Kamati Kuu kufikia maamuzi yake. d) Ndugu Kitila Mkumbo na Samson Mwigamba kwa maneno yao wenyewe wametamka kwamba hawakunishirikisa na sikushiriki kwenye uandaaji wa waraka ambao ndio msingi wa mashtaka haya. Kamati Kuu inao ushahidi huo. 
Wako katika ujenzi wa Chama,
.............................. ......................

Mh. Zitto Zuberi Kabwe (MB).

Soma zaidi Hapa »

KWELI SIASA NI UGONJWA!! TAZAMA WAFUASI WA ZITTO NA WALE WANAOTAKA ZITTO AONDOLEWE WALIVYOZICHAPA NJE YA MAHAKAMA HAPO JANA

0 comments
Dar es Salaam,Tanzania
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imeahirisha kutoa hukumu ya kesi iliyofunguliwa jana na Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Zuberi Kabwe (Chadema), kuhusu ombi la kuitaka Mahakama hiyo kuizuia Kamati Kuu ya Chama hicho, kutomjadili katika kikao ambacho kilipangwa kufanyika leo jijini Dar es Salaam.
Wanachama wa Chadema, wakitwangana nje ya Mahakama Kuu, jijini Dar es Salaam. 
Jaji John Utumwa alisitisha kutoa hukumu hiyo mpaka siku ya Jumatatu saa 4:00 asubuhi.Hata hiyo baada ya Jaji huyo kuahirisha kesi hiyo, nje ya Mahakama hiyo kulikuwa na vurugu kubwa baada ya kundi linalo unga mkono maamuzi ya Chadema kutwangana na kundi linalo muunga Zitto Kabwe.
Mwanachama wa Chadema, anayepinga hoja za Zitto Kabwe, akimtwanga mfuasi wa Zitto Kabwe. 
Hatua hiyo ilisababisha Askari wa Jeshi la Polisi kuingilia kati, huku wakiungana na upande wa Chadema na kuwatwanga marundi wafuasi wa Zitto waliokuwa na mambango kama ilivyokuwa kwa wenzao wa Chadema.
Kesi hiyo ilifunguliwa jana na wakili wa Mbunge huyo Albert Msando huku wakili wa Chadema Tundu Lissu akiweka pingamizi,hata hivyo Jaji John Utumwa wa Mahakama hiyo alitupilia mbali mapingamizi yote yaliyowekwa na Tundu Lissu,

Soma zaidi Hapa »

CHADEMA YATOA AGENDA ZA KIKAO CHA KAMATI KUU HAPO KESHO, ZITTO KIKAANGONI

0 comments

Kutokana na maswali kutoka kwa wanahabari wa vyumba mbalimbali vya habari juu ya agenda za kikao cha Kamati Kuu kesho, Chama kimetoa kauli ifuatayo;
Ni kweli kutakuwa na mkutano maalum wa Kamati Kuu ya chama kesho tarehe 3 Januari 2014 Jijini Dar Es Salaam. Ajenda kuu katika mkutano huo ni tatu;
Mosi: Kupokea taarifa kuhusu mchakato na maudhui ya mabadiliko ya katiba
Kamati Kuu itapokea taarifa juu ya kupitishwa kwa marekebisho ya sheria ya mabadiliko ya katiba 2013, kupitishwa kwa muswada wa kura ya maoni wa 2013, uteuzi wa wajumbe wa Bunge Maalum na kutolewa kwa Rasimu ya Katiba Mpya.
Pili: Kupokea utetezi (wa mdomo) wa wanachama watatu kuhusu tuhuma mbalimbali zilizoelekezwa kwao.
Wanachama hao walishajulishwa makosa yao kwa maandishi na wamewasilisha utetezi wao wa maandishi. Wataitwa kwenye kikao kwa kuzingatia matakwa ya kanuni 6.5.2 (b) na 6.5.2 (d) kupewa nafasi ya kujitetea mbele ya kikao kinachohusika.
Tatu: Mpango Kazi wa Chama kwa mwaka 2014
Mpango Kazi wa chama ni sehemu ya hatua za utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Chama wenye dhima ya kuleta uongozi bora, sera sahihi, mikakati makini na oganizesheni thabiti kwa maendeleo endelevu ya chama na taifa.
John Mnyika
Mkurugenzi wa Mawasiliano

Soma zaidi Hapa »

RASIMU YA PILI YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO IKO HAPA, UNAWEZA KUIDOWNLOAD NA KUSOMA PIA

0 comments
 


RASIMU YA PILI YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YA MWAKA 2013 ILIYOTOLEWA TAREHE 30 DISEMBA 2013
Attachments:
Download this file (RASIMU (Final).pdf)RASIMU (Final).pdf[ ]1073 Kb


Soma zaidi Hapa »

MASTAA KIBAO WA BONGO SASA WAZIDI KUHAMIA CHADEMA, HUYU HAPA MWINGINE

0 comments





ROMA MKATOLIKI WA JIJINI TANGA: Akiongea na Mabest zake Wa Mtaani huko Tanga amesema ana mpango Kuingia Kwenye Uringo wa Kisiasa ili apate nafasi Nzuri ya Kuikosoa Serikali baada ya Muziki wake Kupuuzwa na Viongozi wa Taifa hili. "Naplan Kuzamia Kwenye Mambo ya Politics hivi sasa, By the Way Wiki Ijayo naweza Kuchukua Kadi ya Chadema Rasmi"... Pia amesema Atahakikisha Wasanii Wenzake wanaoimba Muziki wa HipHop akina Kala Jeremiah nao Wanaunda timu ya Maangamizi Kuing'oa CCM Madarakani, ila aliwasihi sana Viongozi wa Chadema Kuwa Karibu nao pale Wanapozushiwa Shutuma za ajabu ajabu Kisa Wamejiunga na Chadema.
Mpaka sasa baadhi ya wanamuziki wa Bongo Fleva waliojiunga na ambao wanampango wa kujiunga na Chama Cha kuwakomboa wanyonge CHADEMA ni Afande Sele wa Morogoro, Joseph Haule ambaye anajulikana kama Prof J, Soggy Doggy na Wengineo wengi.

Soma zaidi Hapa »

SOMA ALICHOPOST ZITTO KUHUSU CHADEMA NA DR SLAA HAPA

0 comments


Kwenye akaunti yake ya FaceBook Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Mhe. Zitto Kabwe ameandika maneno haya :  

"Tatizo la baadhi yetu ni kuishi maisha ya uongo na fitna. Sina tatizo na Dr Slaa. Ni Katibu Mkuu wa chama na amefanya mengi mazuri kufikisha chama hapa.


Sasa hivi watu wanajitahidi sana kuchochea kwa kugeuza maneno ionekane kwamba nina tatizo na Katibu Mkuu wangu. Ziara yangu Kigoma haikuwa 'kumjibu Dr Slaa' kama inavyosemwa. Sina cha kumjibu Katibu Mkuu wangu.
Ninalo jukumu kama mwanachadema ku
toa maelezo kuhusu tuhuma dhidi yangu na pia kuongea na wananchi kuhusu matatizo ya nchi yetu. Hayo sio majibu kwa Dr Slaa kwa sababu ni uonevu kusema Dr Slaa ni Kamati Kuu.

Mimi nitaendelea kutumikia wananchi wa Kigoma na watanzania wote kama mwanachadema na Mbunge. Anayesema naidhoofisha Chadema ni muongo na apuuzwe
."






Soma zaidi Hapa »

KATIKA PICHA : ZITTO ALIPOHUTUBIA KIGOMA MJINI JANA

0 comments

Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, akiwahutubia wananchi wa Kigoma Mjini leo.
Mapokezi ya mbunge Zitto Kabwe.
Zitto akiwashukuru wananchi wa Kigoma Mjini.
(PICHA NA ZITTO KABWE)

Soma zaidi Hapa »

PICHA ZAIDI YA 20: ZITTO ALIPOITIKISA KASULU HAPO JANA, TAZAMA UJIONEE

0 comments






Mh.Zitto Kabwe akiondoka Kasulu,Amezungumzia kuhusu NAMNA CHAMA KINAVYOMSURUBISHA KWASABABU YA HOJA YAKE YA MAHESABU KWA VYAMA VYA SIASA,Mabilioni ya Uswis Na Uwajibikaji wa Viongozi wa serikali pamoja na Wa vyama Vya siasa.\


Kes HERI wana Kasulu,Nitakuja tena kuzungumza nanyi katika jambo lolote lile kabla ya hatua yoyote ile sijaichukua katika Maisha yangu ya siasa.MM ni mtoto wa mama Maskini,Baba Maskini na rafiki zangu ni watu Maskini.
Ninamalizwa na chama changu kwa sababu ya POSHO,NIMEKATAA POSHO LAKINI WAONAO UMIA NI WENGINE.




Zitto anahutubia maelfu ya wananchi



Pia zitto Kabwe amesimikwa hii leo Kuwa MWAMI na wazee wa kasulu



Mamia ya wananchi wakimiminika kwenye uwanja wa Mkutano hapa Kasulu





Mambo ndio hayo KASULU MUDA HUU


Mh.Zitto Kabwe akiwashukulu sana Wanakasulu kwa namna walivyojitokeza kwenye mapokezi hapa kasulu

Ni maelfu ya Wananchi wapo kwenye maandamano ya kumpokea Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mh.Zitto kabwe.

Picha inazungumza wazi namna Msafara ulivyomkubwa sana na umejaa vijana,akina mama na wazee pamoja na watoto wanaotoa sapoti ya kutosha kwa MH.Zitto Kabwe


Maduka Yamefunga watu wote wanaelekea eneo la Mkutano,Hii ni wazi Zitto ni mtu wa watu,Ni mbunge anayekubalika Kigoma na Tanzania


nn

Ushishangae kuona kwenye msafara huu Mkubwa hapa Kasulu Pia hakuna Bendera za chadema,zaidi utaiona moja moja,Ni kwasababu wanakigoma wanasema "ZITTO NI MBUNGE WA KITAIFA,MTETEZI WA WATANZANIA,ZITTO KWANZA,CHADEMA BAADAE"

Mambo yapo hivi hapa Kasulu


Waandishi wa habari pia wapo wengi sana kwaajili yakuchukua matukio na habari

mm

\mm


j

Asanteni wanakigoma


Moja ya Mbango katika mapokezi ya Mh.Zitto Kabwe hapa Kasulu alipopigwa mawe Dr.slaa na kukimbia

Vijana wanatoa sapoti ya Kutosha kwa Mbunge wao zitto


UJUMBE WA CHADEMA"Demokrasia Itashshinda Dhidi ya UHAFIDHINA"



Vijana wakiwa wamejipanga kumpokea Zitto kwenye Vijiji vya Kwanza Kwanza kabla huja fika Kasulu Mjini KM.2 nyuma.

Mambo ndio haya,Wanasema NABII HAKUBALIKI KWAO? Zitto ametikisa Kigoma

Soma zaidi Hapa »
Copyright © 2013. ArtAfropixels Media.com - All Rights Reserved
Customized by: IT XPERTTZ ONE | Powered by: BS
Designed by: Tilabs