MWAKA 2013 : MWAKA WA MAJONZI KWA WASANII
Mwaka 2013 ukiwa unaelekea ukingoni, umekuwa wa huzuni kwenye tasnia ya filamu kutokana na wasanii wengi kupoteza maisha.
Pia katika mwaka huu wa 2013 
kumetokeavifo vya wasanii na kuacha mapengo kwenye tasnia hiyo kama 
ifuatavyo, Januari 2, mwigizaji Juma Kilowoko almaarufu Sajuki alifariki
 dunia, baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Kifo chake siyo tu kiliacha 
pengo bali kilistua watu kutokana na juhudi mbalimbali zilizofanyika 
kuokoa maisha yake, ikiwemo kwenda nchini India kupata matibabu.
Lakini cha kufurahisha aliyekuwa
 mkewe Wastara Sajuki anaendelea kufanya kile alichokuwa akifanya na 
mpendwa mumewe yaani kuendeleza kuigiza, ni matumaini atayafanyia kazi 
yale yote yaliyokuwa yakifanywa na marehemu mumewe.
Januari 8, msanii maarufu wa 
miondoko ya muziki wa mnanda au mchiriku, Omari Omari alifariki dunia 
baada ya kuugua kwa muda mrefu na kuthibitika kuwa alikuwa anaumwa kifua
 kikuu.
Omari Omari ni miongoni mwa vijana waliojipatia umaarufu kupitia muziki huo unaopendwa zaidi maeneo ya uswahilini.
Aprili 17, mwanamuziki mkongwe 
katika miondoko ya taarabu na muziki wa mwambao Fatuma Binti Baraka 
maarufu Bi Kidude alifariki dunia na kuzikwa visiwani Zanzibar, ambako 
ndiyo nyumbani kwao.
Msiba wa Bi Kidude ulihudhuriwa 
na waombelezaji wengi ikilinganishwa na msiba wa mwigizaji Steven 
Kanumba, ambao ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali wakiwemo 
wanasiasa.
Mei 28, mwanamuziki mahiri wa 
muziki wa Hip Hop Albert Mangwair maarufu Mangwea, alifariki dunia 
nchini Afrika Kusini katika Hospitali ya St Heleni Joseph jijini 
Johannesburg na kuzikwa nyumbani kwao Morogoro.
Mwanamuziki huyu, alipata maziko
 ya kutukuka huko nyumbani kwao Morogoro baada ya kuwa na maandano 
ambayo hayakuwahi kutokea , hata mapokezi ya mwili wake ulipofika Uwanja
 wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere yalikuwa ya kihistoria, kutokana na 
watu kufurika na kusukuma gari lililobeba mwili wake hadi maeneo ya 
Tazara jijini Dar es Salaam.
Julai 13, mwanamuziki wa Hip Hop
 Langa Kileo alifariki dunia, Julai 10, mwigizaji Kash maarufu Jaji 
Khadija alifariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa
 amelazwa, aliwahi kutamba na igizo la ‘tamu chungu’.
Septemba
 8, mwigizaji Zuhura Maftaha, maarufu Melisa alifariki dunia, ingawa 
wakati anafikwa na umauti alikuwa anafanya shughuli nyngine baada ya 
kujitoa kwenye masuala ya uigizaji.
Novemba
 11, mtangazaji wa kipindi cha taarabu cha Passion FM, na mwanamuziki wa
 miondoko hiyo Nyawana ‘Matashtiti’ Fundikira, alifariki dunia, nyimbo 
aliyowahi kutamba nayo ni ‘nipo kamili nimejipanga’.
Nyawana alizikwa nyumbani kwao Tabora ikiwa ni kutekeleza kauli yake aliyoitoa akiwa hai kuwa akifa akazikwe kwao.
Imeandaliwa na Kalunde Jamal
Kalunde Jamal
CHANZO: MWANANCHI
 
 

 
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII