WEMA : "MARTIN KADINDA NDIO KILA KITU KWANGU"...DO YOU KNOW WHY?? SOMA HAPA
 
MSANII nyota wa filamu Bongo Wema Isack Sepetu amefunguka kwa kudai kuwa hawezi kuvunja urafiki na meneja wake Martin Kadinda kwa sababu kama kuna kitu chochote cha mafanikio nyuma yake yupo Kadinda.
Wema Sepetu ameuambia mtandao wa FilamCentral kuwa hana rafiki anayejua siri zake zaidi ya meneja huyo ambaye amekuwa akimuongoza vema.
“Kadinda
 ndo kila kitu kwangu, hata akiondoka na kukaa mbali na mimi kwa muda 
mrefu ninapokutana naye tu, nitamweleza kila kitu toka siku ya mwisho 
tuliyoachana, hivyo inakuwa kama sijapoteana naye,yaani ni kama vile nipo naye 
kila siku iendayo kwa Mungu,”anasema Wema.
Msanii huyu ameendelea kusema kwamba hata kampuni yake ya Endless 
Fame film aliifungua kwa msaada wa Kadinda baada ya kumshauri  kuwa kwa hadhi 
yake anastahili kuwa na kampuni na aache kuigiza filamu za watu 
wengine.
 
 
 
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII