Showing posts with label mamtoni. Show all posts

BAADA YA KUTUPIWA LAWAMA ZA KUWAZUIA WASANII WASIHUDHURIE MSIBA WA BABA WEMA, RAY AWAFUNGUKIA WANAOMCHAFUA....SOMA HAPA

0 comments
Mazito!! Msiba wa baba wema wamuweka Ray matatani, adaiwa aliwazuia watu kwenda msibani. Mwenyewe afunguka haya
Klabu ya Bongo Movie ambayo inaundwa na baadhi ya wasanii wakubwa wa filamu nchini imepasuka katikati kisa kikidaiwa kuwa ni lile tamko linalodaiwa kutolewa na mwenyekiti wa klabu hiyo, Vincent Kigosi ‘Ray’ kuwa mwanachama yeyote wa kundi hilo asitie miguu kwenye msiba wa baba mzazi wa mwenzao, Wema Sepetu, marehemu Balozi Isaac Sepetu.
Tukio hilo la katazo lilitokea wakati wa maombolezo ya kifo cha mzee Sepetu kilichotokea Oktoba 27, mwaka huu katika Hospitali ya TMJ kwa ugonjwa wa kisukari ambapo msiba ulikuwa nyumbani kwake, Sinza Mori jijini Dar es Salaam.

Ray alaumiwa sana.

Kufuatia madai hayo, baadhi ya wasanii kutoka klabu ya Bongo movies (majina tunayo) wamekuwa wakitoa lawama zao kwa Ray huku wengine wakidai wamejitoa kwenye kundi hilo kwa sababu halina umoja na limejaa unafiki.
Maneno hayo yalianza kusambaa baada ya Wema kumaliza kumzika baba yake Oktoba 31, mwaka huu mjini Zanzibar.

Wataka kumjadili

Habari za uhakika zinasema kwamba, wasanii waliotangaza kujiengua klabuni humo wameshamuomba Ray aitishe kikao cha dharura kwa ajili ya kuzungumzia hatua yake ya kuwapiga marufuku wasanii hao kutoshiriki msiba wa mzee Sepetu huku akijua wema wa binadamu unapatikana kwenye kushiriki mazishi ya wenzake.
“Kikubwa zaidi ni kwamba, Ray wakati akisambaza zile meseji alisahau kuwa kuna siku Wema aliwahi kuwaalika wasanii wa kundi la Bongo Muvi nyumbani kwake Makumbusho (Dar) wakala na kunywa, mbona hawakugoma kwenda?” alihoji staa mmoja aliyepinga katazo la Ray.

Visingizio vya wanafiki “Tupa Kule”
Maumivu makali zaidi yaliibuka kufuatia baadhi ya wasanii waliotaka kujifanya hawajapata meseji ya Ray ambapo walisema walishindwa kushiriki msiba huo kwa sababu walikuwa ‘shooting’.
“Kuna wasanii walishindwa kuweka wazi kwamba walipokea meseji ya katazo ya Ray, walipopigiwa simu na wenzao kuulizwa kwa nini hawaonekani msibani kwa Wema walisingizia eti wako location wanarekodi!
“Kwa akili za kawaida, mwenzenu kafiwa mnaweza kushikwa na ubize wa kurekodi filamu? Hawa ni wanafiki, walisingizia vile ili ionekane wana hudhuru,” alisema staa mwingine.

Ray afunguka

Baada ya hayo yote hapo tuliamua kumfuatilia kwa karibu sana mwigizaji vicent kigosi ili yujue kama madai haya ni ya kweli aua la na haya ndo baadhi ya mambo aliyoweza kuyasema Ray.
“Kawaida yangu huwa sitetemeshwi wala kuyumbishwa na maneno yamesemwa.mengi cna juu yangu lakini Mungu wa haki ananipigania….kweli nimeamini ukubwa ni jalala na nyota yangu ni kubeba mizigo ya watu. Mtasema sana Lakini Yangu Yananinyokea..." Alimaliza Ray.
Mmmh. Haya sasa mazito. Sisi yetu macho.

Soma zaidi Hapa »

PICHA ZA YANAYOJIRI KWENYE NDEGE INAYOMZUNGUSHA RIHANNA KWENYE TOUR 777......INGIA HAPA

0 comments
Rihanna akiwa na marubani wa ndege ya tour yake
“Are you ready for Mexico? Are you ready for tequiiiiiiila? Sit down, buckle your seat belts, and let’s get drunk,” ni sauti ya Rihanna inayosikika kwenye ndege ya Boeing inayomzungusha kwenye ziara yake aliyoipa jina la 777. 777 maana yake ni siku 7 za tour katika majini 7 ya nchi 7 duniani.
Wakati ndege ikiwa angani mashabiki wa Rihanna waliopata bahati ya kualikwa kwenye tour hiyo pamoja na waandishi wa habari wapatao 150 kinachooendelea ni kula bata na mtungi kwa kwenda mbele.
Katika wakati mmoja safari hiyo iliingia dosari kidogo baada ya mwandishi mmoja kuamua kuvua nguo zake wakati ndege ikiwa hewani na kuamsha kelele na shangwe nyingi kwenye ndege hiyo.
Safari hiyo imeingiwa na dosari baada ya Rihanna kukataa kufanya interview na mwandishi yeyote na kumfanya mtangazaji huyo wa Fox FM ya mjini Melbourne, Australia kuvua nguo zake.
Wengine wanalalamika kuwa Rihanna amekuwa akitumia muda mwingi amejifungia kwenye chumba cha dharura.Pia huduma ya chakuka kwenye ndege hiyo imekuwa ikilalamikiwa na watu hao wanaodai kulishwa vyakula vya ajabu ajabu.
Wengine wanadai kuwa hawana muda wa kupumzika licha kufikia kwenye hoteli za kifahari ambako hulala kwa saa mbili au tatu tu kabla ya kuamshwa tena kuanza safari ya nchi nyingine.
Leo Rihanna atakuwa na show jijini London na tayari ameshaperfom Mexico City, Toronto, Stockhom, Berlin na Paris.
Hizi ni baadhi ya picha za ndani ya ndege hiyo na zile anazotumbuiza kwenye ziara hiyo.





















Soma zaidi Hapa »

HUU NDIO UTAJIRI WA MWANAMUZIKI CELIN DION.....ANAMILIKI NDEGE, NA MIRADI MINGI..

0 comments
MONTREAL, Canada 
CELINE Dion ni mwanamuziki wa Canada, ambaye ana jina kubwa katika medani ya muziki akiamianika kuwa ndiye anayeshikilia rekodi ya kuuza kazi nyingi zaidi za muziki. 

Dion ambaye alianza shughuli za muziki akiwa na umri wa miaka mitano, ana utajiri wa kiasi cha Dola 600 milioni (Sh 50 bilioni za Kenya). 

Mkali huyo anasifika kwa sauti nzuri huku akiwa mahiri wa kuimba muziki wa taratibu, R&B na wakati mwingine classical. 

Aliibuka zaidi mwaka 1990 wakati alipoachia albamu ya Unison na kumfanya ajizolee sifa katika nchi za Marekani, Canada na nchi za Jumuiya ya Madola. 

 Jina la Dion lilijulikana zaidi katika miaka ya 1980 baada ya kushinda mashindano ya kuimba ya Yamaha World Popular Song Festival mwaka 1982 na yale ya Eurovision baada ya kuiwakilisha Uswisi mwaka 1980. 
Hata hivyo, wimbo wa 'My Heart Will Go On' uliotumika katika filamu ya Titanic ndio uliompa chati zaidi katika medani ya muziki. 

Dion anashikilia rekodi ya kuwa mwanamke pekee, ambaye aliuza zaidi ya nakala milioni 200 duniani kote. 

Mwanamuziki huyo ametengeneza utajiri wake kutokana na biashara ya migawaha. Ana migawaha kadhaa nchini Canada iliyo chini ya kampuni yake ya Nickel Restaurants. 
 
Dion anamiliki jumba kubwa katika mji wa Montreal, Quebec ikiwa na thamani ya Dola 29 milioni (Sh 2.5 bilioni za Kenya)
Nyumba huyo ina vyumba sita vya kulala, sehemu ya chakula, jiko, maktaba, gym na sehemu ya kuogelea. 

Pia jumba jingine nchini Ufaransa katika eneo la Montmorency kwenye jiji la Paris likiwa na thamani ya Dola 47 milioni (Sh bilioni nne za Kenya). 
Anamiliki nyumba nyingine katika eneo la Notre-Dame De La Merci lililoko katika mji wa Quebec, Canada. 

Dion anamiliki pia klabu ya Le Mirage, ambayo ina eneo kubwa la kucheza mchezo wa gofu huko Quebec. Aliwekeza kiasi cha Dola 15 milioni (Sh 1.4 bilioni za Kenya) katika klabu hiyo. 
 
Dion anamiliki magari kadhaa lakini mojawapo aina ya Royal Royce Corniche, ambalo limebuniwa na Bill Allen. 

Pia anamiliki ndege aina ya Bombardier, ambayo ina vikolombwezo mbalimbali. Ndege kama hiyo wanayo matajiri Bill Gates na Steven Spielberg. 


The aircraft, operated by Vesey Air on behalf of owner Celine Dion

 

Dion na Rene Angelil walikutana mwaka 1980 wakati Dion akiwa na umri wa miaka 12. Walioana Aprili 17, 1994, katika kanisa la Notre-Dame Basilica mjini Montreal, Quebec.
 

Soma zaidi Hapa »

CHRIS BROWN ARUDIANA NA RIHANNA, AMPIGA CHINI KARRUECHE....SOMA ZAID HAPA

0 comments
BongoNewz
Chris Brown na Karrueche
Chis Brown akiwa na Rihanna
Chris Brown amesema ameachana rasmi na mpenzi wake Karrueche  kwa maelezo kuwa hapendi kumuona akiumia kutokana na urafiki wake na Rihanna.

Brown ametoa taarifa hiyo kwa kusema “Nimeamua kuwa single ili kufocus kwenye kazi yangu. Nampenda sana Karrueche lakini sipendi kumuona akiumia kwasababu ya urafiki wangu na Rihanna.

Ameongeza,”Ni afadhali niwe single ili sote tuwe na furaha na maisha yetu.”

Tangazo hilo la Chris Brown limekuja baada ya Brown na Rihanna kuonekana pamoja kwenye show ya Jay Z huko Brooklyn juzi usiku.

Hata hivyo Karrueche amedaiwa kutoiamini kauli ya Chris kuwa ni rafiki tu na Rihanna na amewaambia marafiki zake kuwa anaamini wawili hao wamekuwa na uhusiano wa kimapenzi.

Mtandao wa TMZ umesema kuwa Karrueche anaona amesalitiwa na mpenzi wake huyo kwakuwa alimwahidi kuwa yeye ndio mwanamke pekee katika maisha yake baada ya kutaka kujua msimamo wake juu ya Rihanna.

Umesema Karrueche alikuwa ameshachezwa ‘machale’ kuwa wapenzi hao wa zamani walikuwa wakimzunguka kwakuwa wiki mbili zilizopita Chris alikuwa amebadilika kwa kwenda klabu peke yake na kumkwepa mpenzi wake.

Vyanzo vimeuambia mtandao huo kuwa Karrueche aliwaambia marafiki zake kuwa alimpenda Chris kwa dhati na alihisi uhusiano ulikuwa imara mpaka pale Rihanna aliporudi tena kwenye picha.


Soma zaidi Hapa »
Copyright © 2013. ArtAfropixels Media.com - All Rights Reserved
Customized by: IT XPERTTZ ONE | Powered by: BS
Designed by: Tilabs