HAWA NDIO MAWAZIRI WANNE WALIOTIMULIWA JANA NA RAIS
RAIS
 Jakaya Kikwete amekubali kuwavua vyeo vyao Waziri wa Mambo ya Ndani ya 
Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, 
Shamsi Vuai Nahodha, Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi , Dk David 
Mathayo na Waziri wa Maliasili na Utalii, Khamisi Kagasheki aliyekuwa 
tayari ametangaza bungeni kujiuzulu. Taarifa hiyo imetolewa na Waziri 
Mkuu, Mizengo Pinda, bungeni baada ya kueleza kuwa ameongea na Rais na 
kukubali kuwavua nyadhifa zao kutokana na ripoti ya Operesheni Tokomeza 
iliyosomwa leo bungeni na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, 
Maliasili na Mazingira, James Lembeli.
 
 



 
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII