MAUAJI HAYA MPAKA LINI?? WATOTO WA DIWANI WA CCM HUKO MBEYA WAUAWA KWA KUNYONGWA..SOMA ZAIDI
Diwani
 wa kata ya Nkangamo Weston Simwelu akifarijiwa na Diwani mwenzake wa 
Kata ya Tunduma Frank Mwakajoka mara baada ya Bw. Simwelu kufiwa na 
watoto wake wawili kwa kuchinjwa na kunyongwa
Katibu Uchumi 
na Fedha wa Kata ya Tunduma akimfariji Diwani wa Nkangamo Weston Simwelu
 ambaye watoto wake waliuawa kinyama kwa kuchinjwa na kunyongwa mjini 
Tunduma.
Mke
 wa Diwani wa kata ya Nkangamo Tumaini Yohana akifarijiwa na ndugu na 
jamaa mara baada ya kutokea kwa mauaji ya kinyama nyumbani kwake ambapo 
mwanaye aliuawa kwa kuchinjwa na mfanyakazi wake wa ndani aliuawa kwa 
kunyongwa.
Jeneza lenye 
mwili wa msichana wa kazi wa Bw. Simwelu, Sista Nyirenge likiwa tayari 
kwa kusafirishwa kwa ajili ya mazishi katika kijiji cha Isansa wilayani 
Mbozi
Diwani wa kata
 ya Tunduma Frank Mwakajoka (kulia) na kiongozi wa mtaa huo Stanslaus 
Malekela wakiwa wanamuongoza Diwani wa Nkangamo Weston Simwelu ambaye 
alipata pigo la kuuawa kwa watoto wawili.
Baadhi ya majirani wa mtaa wa Tazara ambao walifika eneo la tukio kushuhudia mauaji hayo.
Kaka wa marehemu Sista Nyirenge, Mashaka Nyirenge akiwa nje ya chumba cha kuhifadhia maiti kituo cha Afya Tunduma.
Msafara
 kuelekea kijiji cha Isansa kwa ajili ya mazishi yalyotokana na vifo 
vilivyotokana na mauaji ya kinyama yaliyofanyika mjini Tunduma mkoani 
Mbeya.
WATOTO wawili wa Diwani wa Kata ya Nkangamo wilayani Momba mkoani Mbeya 
Weston Simwelu(55) wameuawa kikatili na watu wasiofahamika kwa kuchinjwa
 na kunyongwa baada ya kuvamiwa majira ya saa 8:00 mchana Disemba 19 
nyumbani kwao eneo la Tazara katika mji mdogo wa Tunduma uliopo mpakani 
mwa Tanzania na Zambia.
Mauaji hayo ya kutisha yameteka hisia za wakazi wa eneo hilo kwa madai 
kuwa huenda yanahusishwa na imani za nguvu za giza huku baadhi wakidai 
kuwa yametokana na mgogoro wa kifamilia.
Taarifa za awali katika eneo la tukio zimedai kuwa Diwani huyo alikuwa 
akiishi na mke mdogo aliyefahamika kwa jina la Tumaini Yohana(29) ambaye
 ni mfanyakazi katika halmashauri ya mji mdogo wa Tunduma ambaye wakati 
wa tukio hilo alikuwa kazini.
Imeelezwa kuwa chanzo cha mauaji hayo kinadaiwa ni kitendo cha Diwani 
huyo kuwa mbali na mke mkubwa kwa muda mrefu huku ikidaiwa kuwa mke 
mkubwa amenyimwa mali za mumewe yakiwemo mashamba na nyumba.
Jeshi la Polisi kupitia Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya Barakael 
Masaki amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataja marehemu kuwa ni
 Kalibu Simwelu(6) ambaye aliuawa kwa kuchinjwa shingoni kwa kutumia 
kisu na watu wasiofahamika ambapo mtu mwingine aliyeuawa ni mfanyakazi 
wa ndani aliyetambulika kwa jina la Sista Nyilenda(17).
Kamanda Masaki alisema kuwa Mfanyakazi wa ndani aliuawa kwa kunyongwa 
 kwa kutumia waya wa televisheni iliyokuwepo sebuleni ambapo wauaji 
wanadaiwa kuwavamia na kuwaua kinyama ambapo miili ya marehemu ilikutwa 
sebuleni.
Alisema kuwa wakati wa tukio hilo baba wa watoto hao Bw. Simwelu alikuwa
 shambani katika kijiji cha Kipaka wilayani humo ilhali mama wa mtoto 
Tumaini alikuwa kazini kwake ofisi ya Halmashauri ya Mji mdogo wa 
Tunduma.
Aidha katika tukio hilo Kamanda Masaki alisema kuwa mbali na kufanya 
mauaji hayo, wauaji waliiba mabegi makubwa mawili yenye nguo mbalimbali 
ambayo yalikuwa katika chumba wanacholala watoto.
Kamanda Masaki alisema kuwa kufuatia mauaji hayo watuhumiwa watano 
wametiwa mbaroni ambao ni Gabriel Simwelu(19)Enock Simwelu(23) na Alex 
Simwelu(16) ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya 
Sekondari Mpakani ambao wote ni watoto wa mke mkubwa wa Bw. Simwelu.
Wengine waliokamatwa ni pamoja na Mussa Ngoba(19) mkazi wa mtaa wa Mwaka
 na Patrick Msigwa(18) mkazi wa mtaa wa Majengo na kwamba miili ya 
marehemu imehifadhiwa katika kituo cha Afya Tunduma.
Picha na habari kwa hisani ya Mkwinda Blog
 
 
 
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII